Hatimaye, Njia Bora Ya Matumizi Ya Mitandao Ya Kijamii Imeanza Kutumika.

Ni masaa mangapi unatumia kila siku kuzurura kwenye mitandao ya kijamii?

Unapaswa ufahamu hili miaka 20 iliyopita, kabla ya mitandao ya kijamii na simu janja hazijaingia kwenye maisha ya watu, mtandao ulipewa nafasi ya kufanya makubwa  na hakuna aliyeweza kufikiri ingekuja na madhara makubwa kwa watumiaji wake.

Lakini miaka 10 baadaye, mambo yakawa yamebadilika kabisa.

Simu janja zikawa sehemu ya maisha ya kawaida ya watu na mitandao ya kijamii ikawa njia kuu ya mawasiliano na kupashana habari.

Hatari kubwa ambayo imeibuka ni usumbufu mkubwa ambao umeletwa kwenye maisha yako na simu hizi janja pamoja na mitandao ya kijamii.

Imekuwa vigumu sana kupata utulivu na umakini wa kuweka kwenye yale mambo muhimu ya maisha yako.

Kila mara unapata msukumo wa kuingia kwenye mitandao hii, kushirikisha kuhusu maisha yako au kuangalia nini kinaendelea kwenye maisha ya wengine.

Imefikia hatua ambayo unajishangaa mwenyewe, una akili kubwa sana ya utambuzi na kufanya maamuzi lakini unashindwa kujizuia kutumia simu janja na mitandao ya kijamii bila kikomo.

Tatizo hili limezidi kukua na sasa madhara yake yanakwenda zaidi kwa vijana wanaokulia katika kizazi hiki, wengi wanakosa muda wa kutengeneza mahusiano imara ya kijamii, ya kuwa na watu ana kwa ana kwa sababu muda wao mwingi wanautumia kwenye mitandao ya kijamii.

Kazi pia zimeathirika sana na mitandao hii, wewe ni mmoja kati ya wengi mnaokiri ufanisi na uzalishaji wako kushuka kutokana na matumizi makubwa ya mitandao hii ya kijamii.

Imegundulika njia bora ya kutatua changamoto hii, ni kutumia falsafa bora ya matumizi ya mitandao ya kijamii, ambayo ina manufaa kutokana na madhara ya mitandao hii.

 Falsafa hii haibadili kitu kimoja kwenye matumizi yako ya simu janja na mitandao ya kijamii, bali inabadili mfumo wako mzima wa maisha na jinsi unavyoichukulia na kuitumia mitandao hii.

Rafiki unaifahamu falsafa bora ya matumizi ya mitandao ya kijamii iliyonisaidia mimi na maelfu ya watu?

Rafiki kama hauifahamu  na hujaanza kuitumia nakushauri usome SURA YA NNE(4) ya kitabu kinachoitwa EPUKA UTUMWA WA KIDIJITALI, ukurasa wa 98.

Na kama mpaka sasa bado uja pata nakala yako ya kitabu wasiliana na namba 0752977170, utaletewa au utatumiwa popote ulipo ndani ya AFRIKA MASHARIKI.

Unavyozidi kuchelewa kuchukua hatua ndivyo unavyozidi kupoteza rasilimali muda.

Kupitia kitabu hiki utajifunza mambo saba(7) makubwa ambayo yatakufanya uwe huru na  kuondokana na usumbufu unao kuingiza kwenye utumwa.

Moja utajifunza jinsi ubongo wako unavyofanya kazi na namna teknolojia mpya zinavyotumia ubongo huo kukufanya kuwa mtumwa.

Teknolojia mpya zimetengenezwa kwa namna ambayo zitajenga uteja/uraibu kwenye ubongo wako.

 Kwa kujua njia hiyo utaweza kuepuka kuingia kwenye utumwa wa teknolojia hizo.

Mbili utajifunza kuhusu zama tunazoishi sasa, zama za maarifa na taarifa lakini ambazo zimegeuka kuwa zama za usumbufu.

Utajifunza zama hizi za usumbufu zimetengeneza makundi makubwa mawili, wachache wanaonufaika sana, kama Mark Zuckerberg ambaye ni mmiliki wa Facebook na wengi ambao ni kama watumwa wa wachache hao wanaonufaika.

Ndani ya sura hii utajifunza jinsi ya kufikia viwango vya juu vya ufanisi.

Tatu utajifunza jinsi ya kujua kama tayari umeshanasa na kuwa mtumwa wa teknolojia hizo mpya.

 Unaposoma hapa unaweza kusema wewe hujawa mtumwa, unatumia kwa kupanga mwenyewe, lakini nikuambie kitu kimoja, kwa sehemu kubwa sana umeshakuwa na utaziona dalili kwa kusoma kitabu hiki.

Nne utajifunza jinsi ya kuondoka kwenye utumwa wa kidijitali ambao umeshaingia.

 Baada ya kuona jinsi ambavyo umenasa kwenye utumwa huo, utajifunza njia za kujinasua.

Hapa utajifunza jinsi ya kuizidi ujanja simu janja yako.

Tano utajifunza falsafa mpya ya kuendesha maisha yako kwa uhuru katika zama hizi za usumbufu.

Pamoja na kujifunza kuhusu zama hizo na jinsi ya kuondokana na utumwa wake, usumbufu wake hautaisha, teknolojia mpya zinaendelea kugunduliwa kila siku na zikiwa na ushawishi mkubwa.

Hivyo unahitaji kuwa na falsafa unayoitumia kuchagua huduma za kidijitali utakazochagua kutumia kwa manufaa yako.

Sita utajifunza jinsi ya kutumia akili yako kuvunja uraibu wowote ambao umeshajijengea. Kama tulivyoona, huduma za kidijitali zinatumia jinsi ubongo unavyofanya kazi kukuingiza kwenye utumwa.

 Hivyo wewe unapaswa kuutumia ubongo wako vizuri kuondoka kwenye utumwa huo.

Saba utajifunza sababu kumi kwa nini unapaswa kuondoka kwenye mitandao yote ya kijamii sasa hivi. Hizi ni sababu ambazo zimechambua jinsi matumizi ya mitandao ya kijamii yalivyo na athari kwenye akili yako, utulivu wako, mahusiano yako, uchumi wako na hata imani yako. Kwa kuzijua sababu hizi kumi, utajionea mwenyewe jinsi ulivyorudi nyuma tangu umeanza kutumia mitandao hiyo na hivyo kuachana nayo ili kuepuka madhara yake.

Mwisho kabisa utajifunza njia za kutumia kufanya maamuzi iwapo utumie huduma ya kidijitali.

Utajifunza jinsi ya kutumia vigezo vitatu vya AFYA, UTAJIRI na HEKIMA katika kuchagua na kutumia teknolojia mpya, ambazo zitakuwa na manufaa kwako badala ya kukufanya mtumwa.

Tuko kwenye vita, adui mkuu anajua yuko vitani ila wanaolengwa hawajui.

Hivyo unapaswa kuwa na maandalizi mazuri ya kupambana na vita hii ili uweze kutoka salama na siyo kuwa mfungwa.

Pata na usome kitabu cha EPUKA UTUMWA WA KIDIJITALI ili upate mbinu za kupambana kwenye vita hii na kutoka ukiwa mshindi. Kitabu hiki kimechapwa kwa nakala ngumu (hardcopy).

Kitabu kinauzwa TSH elfu 20 (20,000/=) na ili kukipata wasiliana na 0752 977 170 na utaletewa au kutumiwa kitabu popote ulipo Tanzania na Afrika Mashariki.

 Kwa sababu ya maombi ya watu wengi Leo tunatoa OFA kwa waatu ishirini na tano(25) wa kwanza, ukinunua LEO kitabu cha EPUKA UTUMWA WA KIDIJITALI, utapata fursa ya kujiunga na chaneli ya SOMA VITABU TANZANIA.

Unachotakiwa kufanya ni kutuma ujumbe mfupi unaosomeka “NIUNGE” kwenda namba 0752977170, baada ya kununua kitabu chako.

Vigezo na masharti kuzingatiwa.

MUHIMU; Kama utanunua na kusoma kitabu hiki na ukaona hakina manufaa yoyote kwako, unaruhusiwa kukirudisha na ukarejeshewa fedha zako.

Hivyo chukua hatua sasa, huna cha kupoteza lakini una mengi ya kupata, yatakayokuweka huru kwenye zama tunazoishi sasa.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Related Post