Unazo Sekunde 5! Kila Mtu Ni Muuzaji.

Unazo Sekunde 5! KILA MTU NI MUUZAJI.

Rafiki Yangu Mkubwa, hata wewe ni muuzaji,

Waliofanikiwa sana wamekuwa ni wauzaji wazuri sana.

Mfano wa majina ambayo yatakushangaza ni ; Steve Jobs, Martin Luther King, Jr, Nelson Mandela, Sir Alex Ferguson,
LeBron James, Richard Branson na Oprah Winfrey.

Kupitia majina hayo, umejionea mwenyewe kwamba mtazamo wako kwenye mauzo ni tofauti na uhalisia.

Umeona jinsi ambavyo wale waliofanikiwa sana wamekuwa ni wauzaji wazuri wa kile
walichokuwa nacho Watoto wadogo wanapoulizwa wanataka kuwa nani wakiwa wakubwa,

… huwa wanataja taaluma kama udaktari, uanasheria, ualimu, uhasibu au wachezaji.

Huwezi kumsikia mtoto mdogo akisema akiwa mkubwa anataka kuwa mtu wa mauzo.

Mauzo huwa haionekani kama tasnia kamili na yenye mafanikio.

Mauzo imekuwa ikichukuliwa kama tasnia ya watu waliokosa kitu kingine cha kufanya.

Huu ni mtazamo usio sahihi ambao umewakwamisha wengi kwenye mauzo.

Ukweli ni kwamba, kwa chochote kile ambacho mtu anafanya, mafanikio yake yanategemea sana uwezo wake wa kuwashawishi wengine kukubaliana naye.

Na zoezi la kuwashawishi wengine wakubaliane na wewe ndiyo mauzo.

Haijalishi ni kitu gani unachotaka wengine wakubaliane na wewe, UNAUZA.

Kwa kifupi kila mtu kuna kitu ambacho anauza.

Hivyo kuona tasnia ya mauzo kama kitu cha watu walioshindwa siyo sahihi.

Mauzo ni kitu ambacho kila mtu anafanya kwenye maisha yake na mafanikio ya mtu yanategemea na jinsi anavyokuwa bora kwenye mauzo.

Watu wengi sana wanashindwa kwenye maisha kwa sababu ya kukosa ushawishi kwa wengine.

Haijalishi una kitu kizuri kiasi gani,

kama huwezi kuwashawishi wengine wakubaliane na wewe, huwezi
kufanikiwa.

Rafiki Yangu Nakuahidi Utakuwa Mtaalam Wa Mauzo.

Watu wengi huwa wanajikuta kwenye mauzo siyo kwa kupanga, bali kama ajali.

Labda unakuwa umeanzisha biashara na kulazimika kufanya mauzo.

Au umekosa cha kufanya na kulazimika kuwa wakala wa mauzo wa bidhaa au huduma fulani.


Ukweli ni kwamba kila mmoja wetu ni muuzaji.

Japo tasnia ya mauzo imekuwa inapewa jina na mtazamo mbaya, hakuna mtu aliyefanikiwa
ambaye hakuwa muuzaji mzuri.

Ni uwezo wa kuuza mawazo, bidhaa
na huduma ndiyo umewasaidia watu mbalimbali kuweza kufika kwenye kilele cha juu kabisa cha mafanikio.

Rafiki Yangu, Uwezo wa kuwa Mtaalamu wa Mauzo Upo Ndani Yako.

Ulichobakiza Mpaka Sasa Ni Wewe Kuchukua Hatua Ya Kusoma Kitabu Hiki Cha CHUO CHA MAUZO,

Nakuamini utakuwa Muuzaji Bora Kuwahi Kutokea, Ni Swala La Muda Tu!

Rafiki Yangu Kama bado hujakipata usikonde  piga simu kwenye namba hii 0752977170.

Utaletewa au utatumiwa popote ulipo.

Bado kinapatikana kwa bei ya siti ya bus ambayo ni Tshs 29,999Tu! Badala Ya Siti Ya VIP 50,000.

Karibu Sana.

Ni Mimi Rafiki Yako Ninayekupenda Na Kukujali Sana.

Bwana Amiri Ramadhani |CopywriterOfSomaVitabuTanzania|| Mjasiriamali Mjanja|

One thought on “Unazo Sekunde 5! Kila Mtu Ni Muuzaji.”

  1. Jinsi gani mtazamo wa mauzo kama njia ya kazi ya kurudi nyuma inaweza kubadilishwa, hasa kwa kuzingatia jukumu lake la msingi katika kushawishi wengine na kufikia mafanikio katika jitihada mbalimbali? Tembelea yetu Telkom University

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Related Post