HAKIKISHA! Siku Zote Unapopambana Na Changamoto Yoyote Ile Usisahau Kutumia Mbinu Hizi Muhimu Zenye Matokeo Ya Haraka…!

HAKIKISHA! Siku Zote Unapopambana Na Changamoto Yoyote Ile Usisahau Kutumia Mbinu Hizi Muhimu Zenye Matokeo Ya Haraka…!

Rafiki yangu mpendwa,

Katika maisha lazima ujue kila wakati unaweza kukutana na changamoto.

Na watu wanasema kila ukitoka kwenye changamoto moja utaingia kwenye changamoto nyingine, duniani hapa kama hauko kwenye changamoto basi utakuwa umetoka kwenye changamoto au unaelekea kwenye changamoto nyingine.

Shida sio changamoto unazokutana nazo, tatizo kubwa ambalo watu linawakabili ni namna ya kushughulika na changamoto ambazo zile zinatokea katika maisha yao.

Na Leo lingependa nikwambie namna ambavyo unaweza kutoka kwenye changamoto yoyote inayokukabili, inawezekana leo upo kwenye changamoto kwenye taaluma yako inawezekana leo upo kwenye changamoto ya mahusiano yako au upo kwenye changamoto ya kiuchumi, au upo kwenye changamoto ya kazi, kazi unayofanya au eneo lako la kiofisi au kwenye biashara yako.

Bila kujali upo kwenye changamoto ipi kuna maeneo manne ukiweza kuyazingatia yatakusaidia sana kutoka kwenye changamoto yako tena kwa haraka.

Kumbuka tena washindi ni wale ambao wakipita kwenye changamoto wanaondoka kwenye changamoto zao kwa haraka sana bila kuchelewa.

Jambo La Kwanza; Ambalo unatakiwa kulifahamu katika maisha yako ni kwamba unapopitia changamoto USIKUBALI ile hali ya kujiambia changamoto yako ni SPESHO.

Changamoto SPESHO, maana yake ni kuna watu wanafikiri wanapopitia matatizo ni wao ndio wa kwanza kupitia katika matatizo hayo na hakuna mtu mwingine yeyote aliyepitia katika changamoto hiyo.

SI KWELI, ukiwa na fikra ya namna hiyo utashindwa kabisa kukabiliana na changamoto yako.

Changamoto yoyote leo unayokutana nayo, cha kwanza ambacho ningependa nikuambie. Kuna mtu ameshawahi kukutana na changamoto kama hiyo, na katika wale waliokutana na changamoto kama hizo hakika wako ambao wameshinda hizo changamoto.

Lakini kuna mtu leo anapitia changamoto kama ya kwako na hakika anaweza akashinda pia, wewe ukajua na kufikiri kwamba changamoto yako ni SPESHO na hakuna mtu ambaye anachangamoto kama ya kwako, hakika hautavuka, hautatoka katika hiyo changamoto.

Kuna watu ambao wakipitia matatizo wanaona changamoto yao hakuna mtu mwingine yeyote mwenye nayo. Wanaona kama lile tatizo ndio mara yao ya kwanza wanalipitia duniani yaani ni kama limevumbuliwa hakuna mtu mwingine ambaye amekutana nalo.

SI KWELI, usikubali hata siku moja kwamba changamoto yako ni SPESHO hakuna mtu mwenye changamoto kama hiyo, ukiwa na fikra kwamba changamoto yako ni spesho , hautapata uvumbuzi mapema na utaona hakuna msaada.

Cha kwanza kabisa kataa fikra inayokuambia changamoto yangu ni spesho hakuna mtu kama mimi, mtu aliyopo kama mimi, hakuna mtu aliyepata matatizo kama mimi.

SI KWELI, wako wengi na wameshinda na wewe unaweza kuishinda.

Jambo La Pili; Unalotakiwa kulifahamu ni kwamba changamoto yoyote unayopitia ni SAIZI YAKO, watu wengi ambao changamoto zinawazidi sio kwa sababu wanashindwa kuzitatua kwa sababu walikata tamaa.

Ningependa nikuambie changamoto yoyote ile unayokabiliana nayo leo ya KIFEDHA, ya KIMAHUSIANO, ya KITAALUMA, KAZINI KWAKO au kwenye BIASHARA, inawezekana kabisa umekosa usingizi kabisa kwa sababu ya changamoto inayokukabili.

Ninachotaka nikuhakikishie ni kwamba changamoto hiyo unayokutana nayo leo ni SAIZI YAKO.

Ukiwa na fikra ya namna hiyo tafsiri yake ni kwamba utafanya kila unachoweza, kuweza kukabiliana nayo, unapokubali kwamba changamoto hii ni SAIZI YAKO. Unaulazimisha ubongo wako kutafuta suluhisho unaposema changamoto hii imenizidi umri unauambia ubongo wako ila tu kwa sababu hakuna kitu ninaweza kufanya.

Ninachotaka kukuambia ni kwamba changamoto ni saizi yako, ya mambo unayopitia leo.

Jambo La tatu; Ambalo ni la msingi sana, kulijua katika kutoka kwenye changamoto unayokutana nayo ni kujua katika kila changamoto KUNA MLANGO WA KUTOKEA, kuna njia za wewe kutoka kwenye changamoto ukweli ni kwamba hukuuona huo mlango wakutokea.

Ukweli ni kwamba haujaona njia za kutoka kwenye changamoto zinazokukabili haimaanishi kwamba changamoto yako imekosa suluhisho, kuna suluhisho kwenye changamoto yako inawezekana haujaiona ndio maana tunasema kama leo unapitia changamoto usikubali tu kukaa nyumbani, usikubali tu kukaa ndani, usikubali kujifungia, tafuta watu uzungumze nao, nenda mahali toka nje fuatilia kitu fulani utapata suluhisho.

Hakuna changamoto ambayo haina suluhisho katika maisha hata ya kwako, iwe inawezekana umefika sehemu unasema kwamba nimejaribu kila nilichofanya kupata suluhisho.

SI KWELI, changamoto uliyonayo ina suluhisho kama hutokata tamaa utapata suluhisho ya changamoto yako.

Jambo La Mwisho; Ambalo litakusaidia kutoka kwenye changamoto ambayo inakukabili sasa hivi kwa haraka sana nikijua kwamba changamoto zinapokuja saa zingine zinatuepusha na mabaya makubwa ambayo hatuyaoni.

Kuna watu wengi sana wanapitia changamoto za mahusiano na kusema yule nilimpenda sana, nikajitolea na leo hayupo tena kwenye maisha yangu, kuja kugundua kwamba hapana kumbe ni sababu ya wao kupata watu sahihi zaidi, kuna watu walifukuzwa kazi, kuna watu waliondolewa ofisini kwa kudhalilishwa lakini leo wanamiliki makampuni yao au wengine wamepata kazi kubwa zaidi.

Kwa hiyo kila wakati unapokutana na changamoto uwe na jicho la ziada la kuangalia usiangalie kile tu ulichokosa lakini pia kuna kitu ambacho kiko leo.

Kwa nini inakuwa hivyo mara nyingine tukiambiwa tuache vya sasa hivi tulivyonavyo ili tupate bora, tulivyoandaliwa mbele yetu hatutakuwa tayari kufanya maamuzi magumu ya namna hiyo kwa sababu yanatuumiza, lakini changamoto zinakuja pia kutuepusha na mabaya ambayo kwa macho ya kawaida hatuyaoni, ndio maana changamoto unayopitia leo ni mbaya na inakuumiza sana.

Lakini kesho utamshukuru mungu na kusema afadhali nimepitia hii changamoto. Kwa sababu imenisaidia kuwa hivi nilivyo sasa.

Inawezekana leo unapita katika changamoto yako.

Ningependa uniandikie hapo chini unapitia changamoto gani na mimi nitajaribu kukushauri zaidi ni namna gani unaweza kutoka kwenye hiyo changamoto inayokukabili.

Rafiki Yako Mpendwa Ninayekujal Na Kukuthamini Sana.

Sir Rama.

Tuendelee Kujifunza….

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Related Post