Jinsi Ya Kuzivuta Fedha Kuja Kwako…

 Jinsi Ya Kuzivuta Fedha Kuja Kwako…

Rafiki Yangu Mpambanaji,

Leo ni siku ambayo unakwenda kujifunza jinsi ya kuzivuta fedha kuja kwako.

Endapo utasoma makala hii mpaka mwisho na kuielewa.

Utajiri ni kitu ambacho kila mtu anakipenda,

…kwa sababu fedha ni hitaji muhimu kwenye maisha yetu ya kila siku.

Ila kwenye jamii yoyote ile, ni wachache sana wanaofikia utajiri,

…kwa sababu wachache hao kuna siri wanazozijua kuhusu fedha na utajiri, ambazo wengi hawazijui.

Je ungependa kuzijua siri hizo ili na wewe uweze kufikia utajiri kwenye maisha yako?

Kama jibu ni ndiyo basi kaa hapa, maana umefika mahali sahihi.

Kabla hatujaendelea nikukumbushe kwamba kinachowatofautisha tajiri na masikini siyo umri,

… kuna matajiri vijana na wazee, na wapo masikini vijana na wazee.

Na wala siyo kiwango cha elimu, kuna matajiri ambao hawajasoma kabisa na waliofika viwango vya juu ambao ni masikini.

Na wala hawatofautiani kwa rangi, kabila au jinsia.

Kwenye kila kundi la watu, kuna matajiri na masikini.

Hivyo kitu pekee kinachowatofautisha matajiri na masikini ni kile wanachojua na hatua wanazochukua.

Hayo mawili tu, WANACHUJUA na WANACHOFANYA.

Hiyo ina maana kwamba kama ukijua kile matajiri wanachojua na ukifanya wanachofanya, lazima na wewe uwe tajiri.

Je upo tayari kujua, ili uweze kufanya na utoke hapo ulipo sasa?

Kama jibu ni ndiyo, basi karibu ujue kile matajiri wanajua na kikusaidie kufanya wanavyofanya na uwe tajiri.

Kuna maeneo kumi kuhusu fedha ambayo matajiri wanajua tofauti na masikini na hatua wanazochukua kwenye maeneo hayo ni tofauti na wanazochukua masikini.

Eneo la kwanza ni dhana halisi ya fedha, wanavyoichukulia fedha matajiri ni tofauti kabisa na masikini.

Eneo la pili ni kipato, matajiri wanajua jinsi ya kuingiza kipato hata wakiwa wamelala.

Eneo la tatu ni matumizi, masikini ni wazuri kwenye matumizi na hapo ndipo wanaachwa nyuma.

Eneo la nne ni madeni, matajiri wanajua madeni mazuri na mabaya na wanayatumia kwa umakini mkubwa.

Eneo la tano kutengeneza kipato kisicho na ukomo, vipato vya matajiri huwa havina ukomo.

Eneo la sita ni kuweza kuendelea kuingiza kipato hata wanapokuwa wamestaafu, matajiri wanajua kujiandaa kwenye hilo mapema.

Eneo la saba ni kodi, matajiri huwa wanalipa kodi ndogo kuliko masikini na wanafanya hivyo kisheria kabisa.

Eneo la nane ni kulinda utajiri usipotee, kupata utajiri ni jambo moja, kuuliza usipotee ni jambo jingine ambalo wengi hawalijui.

Eneo la tisa kuwaandaa watoto kuridhi na kukuza utajiri waliotengeneza, matajiri wa kweli wanawaandaa watoto wao vizuri ili mali walizopata zisipotee.

Eneo la kumi ni utoaji, matajiri wanajua utajiri wao siyo wao peke yao, hivyo wamekuwa wanatoa kwa jamii na wanapotoa ndivyo wanavyopata zaidi.

Umepata kwa ufupi sana mambo haya kumi, ili uweze kuyajua kwa kina na ujue hatua za kuchukua,

…karibu upate kitabu chako cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA.

Kitabu hicho kimeyajadili mambo hayo kumi kwa kina pamoja na mifano mbalimbali na kukupa hatua za kuchukua ili uweze kufika kwenye utajiri mkubwa.

Ukisoma Leo kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, na kufanyia kazi utakayojifunza basi kuanzia leo utaweza kuzivuta pesa kuja kwako.

THAMANI Ya Kitabu Ni $23 (Dola 23)  ila kwasababu leo ni siku yako muhimu sana,

Utakipata kwa zawadi ya Tsh elfu 19,950 Tu, l

Kupata kitabu chako sasahivi tuma meseji Inayosomeka “FEDHA”kwa WHATSAPP Namba 0752 977 170 ,

…na utaletewa au kutumiwa kitabu popote ulipo Tanzania na Afrika Mashariki.

MUHIMU; Zawadi hii ni kwa siku ya leo tu.

Kama utanunua na kusoma kitabu hiki na ukaona hakina manufaa yoyote kwako, unaruhusiwa kukirudisha na

ukarejeshewa fedha zako. Hivyo chukua hatua sasa, huna cha kupoteza lakini una mengi ya kupata.

Safari yako ya kuelekea kwenye utajiri imezuiwa na kile usichojua na hatua usizochukua.

 Pata kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA leo hii na ujue yaliyo sahihi na hatua za kuchukua kuelekea kwenye utajiri.

Kila Lakheri,

Karibu, www.somavitabu.co.tz

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Related Post